Askari polisi wa Kituo cha Babati mkoani
Manyara, Boniface Masunga (32) amefariki dunia baada ya baiskeli aliyokuwa
akiendesha wakati akielekea kazini kumgonga mtembea kwa miguu
Baada ya kumgonga mtu huyo, askari huo
aliangukia kichwa na kufariki dunia papo hapo
Akizungumza leo Jumamosi Machi 24, 2018,
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Manyara, Agostino Senga amesema tukio hilo limetokea
jana katika barabara kuu ya Babati-Singida.
Amemtaja aliyegongwa kuwa ni Awadhi Ashraf (20) mkazi wa mjini Babati na kwamba, chanzo cha ajali hiyo ni Ashraf ambaye ni fundi ujenzi kuingia barabarani bila kuchukua tahadhari
"Huyo fundi alikuwa anaingia kwenye barabara kuu ya lami bila kuchukua tahadhari, hivyo akagongwa na baiskeli aliyokuwa anaendesha polisi huyo," amesema Kamanda Senga
"Tukio hilo lililotokea ghafla sana
kwani alivyomgonga aliangukia kichwa na kuanza kutokwa damu masikioni.”
Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda wa ajali
hiyo walishangazwa na ajali hiyo kwani hawajawahi kuona mtu akagongwa na
baiskeli na mwendeshaji kufa
Mkazi wa eneo la Sawe mjini Babati, Mariki John amesema tukio hilo ni la kushangaza kwani askari huyo japo alikuwa mdogo kiumri, lakini baiskeli imesababisha kifo chake.
ASKARI POLISI AFARIKI DUNIA BAADA YA KUMGONGA MTEMBEA KWA MIGUU.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 24, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment