CHADEMA NA UKAWA WASHINGTON WASAINI MIKATABA

Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kanda ya kaskazini kimesaini hati ya mashirikiano Matano na chama  cha  CHADEMA DIASPORA kilichoppo WASHNGTON SEATTLE nchini Marekani lengo likiwa ni kujenga misingi ya chama kupitia maelewano ya kupeana fursa mbalimbali zikiwemo  za kibiashara, Masoko , Siasa na jamii zitakazowezesha kuking'oa madarakani chama cha mapinduzi 2020.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha Machi 19, Katibu wa CHADEMA  kanda ya kaskazini Amani Golugwa amesema mambo mengine waliokubaliana ni masuala ya uenezi wa chama katika kukabiliana na chaguzi mbalimbali zijazo,ikiwemo masuala ya vipeperushi

Golugwa amesema mashirikiano hayo yamelenga kuimarisha misingi ya chama ndani na nje ya nchi hasa katika nyanja za kiuchumi ,pia kuwaunganisha wafuasi wa chadema waliopo nje ya nchi  katika kusafiri pamoja na Utoaji na usambazaji wa habari

Kwa upande wake kiongozi wa chama cha chadema, Diaspora Washngton Seattle nchini Marekani ,Pascal Kikubi amesema  mashirikiano hayo ni muhimu sana hasa katika kipindi hiki cha siasa za ushindani
Ameongeza kuwa hapo awali kulikuwa na mashirikiano hafifu huku baadhi ya viongozi wa chadema  wakifika Marekani na kutoa Ahadi mbalimbali lakini mwisho wa siku kunakuwa hakuna utekelezaji,jambo ambalo wamekubaliana kutojirudia

Amesema baadhi ya mambo waliokubaliana ni masuala ya  kisiasa ,kijamii, kubadilishana usafir
CHADEMA NA UKAWA WASHINGTON WASAINI MIKATABA CHADEMA NA UKAWA WASHINGTON WASAINI MIKATABA Reviewed by KUSAGANEWS on March 20, 2018 Rating: 5

No comments: