Mvua yaua mwanafunzi Kibohehe

Mwanafunzi mmoja wa darasa la sita wa Shule ya Msingi Kibohehe, iliyoko wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, amefariki dunia na wengine watano kujeruhiwa, baada ya kuangukiwa na ukuta.
Mwanafunzi huyo wa kiume ameangukiwa na ukuta wa chumba chadarasa baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha leo mchana

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya Simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah, amesema mwanafunzi huyo alikuwa akiingia kwenye kipindi cha dini na ndipo alipokutana na ajali hiyo ya ukuta na kupoteza maisha

“Mvua ilinyesha na upepo mkali, jengo moja la darasa likadondoka na kumwangukia mtoto huyo ambaye alikuwa akiingia kwenye kipindi cha dini,”amesema Issah

Aidha Kamanda amesema, majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Hai kwa ajili ya matibabu na kwamba uchunguzi zaidi wa tukio hilo
Mvua yaua mwanafunzi Kibohehe Mvua yaua mwanafunzi Kibohehe Reviewed by KUSAGANEWS on February 21, 2018 Rating: 5

No comments: