MAKAMU WA RAISI AAHIDI KUSHUGHULIKIA WAKUU WA WILAYA

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kuwa atawashughulikia wakuu wa wilaya ambao watashindwa kukomesha vitendo vya wanafunzi wa kike kupewa mimba.

Amesema kuwa yeye kama kiongozi mkuu wa juu mwanamke, atahakikisha anapambana na watu wote wanaowapa mimba watoto wa kike wakiwa bado shuleni, huku akiwaonya madereva pikipiki (bodaboda).
Mama Samia ametoa kauli hiyo jana kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi uliofanyika katika viwanja vya Nguzo Nane mjini Maswa mkoani Simiyu.
Amesema  atahakikisha anawashughulikia wakuu wa wilaya wote nchini ambao hawataonyesha jitihada zao za kuhakikisha wanapambana na wale wote wanaowapa mimba watoto wa kike
“Mimi kama kiongozi wa juu mwanamke ni lazima macho yangu yawe makini kuangalia na kuwashughulikia wale wote ambao wanawaharibia  malengo kusudiwa watoto wa kike…na kuonyesha kuwa niko makini nitaanza na wakuu wa wilaya wasiowajibika na hilo,’’ amesema Mama Samia.Amesema  kuwa serikali  haiwezi kuwafumbia macho wale wote wanaoharibu maisha ya watoto wa kike halafu wakaachwa tu bila sheria kali kuchukuliwa dhidi yao.

Aliongeza kuwa Serikali yake imekuwa ikijitahidi kutoa  fedha nyingi kila mwezi katika sekta ya elimu ili kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bure hivyo hatarajii kuona watoto wa kike wanaishia njiani pasipo kutimiza ndoto zao
Awali akimweleza Makamu wa Rais Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Seif Shekilage alisema wilaya yake imekuwa na tatizo kubwa la mimba kwa watoto wa kike na kwa kipindi cha Desemba 2017 hadi sasa tayari matukio ya mimba yamefikia 20
Shekilage amesema kati ya kesi 20 zilizofunguliwa kesi mbili tayari zimeshatolewa hukumu na watuhumiwa wamefungwa kifungo cha miaka 30 jela
Dk Shekilage amesema kuwa wilaya yake imekuwa ikijitahidi kuhakikisha tatizo la mimba linaisha kwa kutoa elimu kwa watoto wa kike na jamii ikiwa sambamba na kuwachukulia wale wanaobainika kuwapa mimba wanafunzi

“Katika wilaya yangu tunajitahidi kuhakikisha suala la mimba tunalipunguza…mimi binafsi nafuatilia sana wale waharibifu wanaoharibu maisha ya watoto wa kike,’’ amesema

Pia amemuhakikishia Makamu wa Rais kupambana na wote wanaowaharibia wanafunzi maisha yao kwa kuwapa mimba ili watoto hao wa kike waweze kufikia malengo.
Akiwa wilayani Itilima Makamu wa Rais aliahidi kujenga hospitali ya wilaya, ambapo Mbunge wa Jimbo hilo Njalu Silanga (CCM) alisema ukosefu wa hospitali hiyo umekuwa kero kwa wananchi wake.




MAKAMU WA RAISI AAHIDI KUSHUGHULIKIA WAKUU WA WILAYA MAKAMU WA RAISI AAHIDI KUSHUGHULIKIA WAKUU WA WILAYA Reviewed by KUSAGANEWS on February 21, 2018 Rating: 5

No comments: