MTOTO WA MIAKA SITA AFARIKI AKIOMBEWA KUTOA MAPEPO

Mtoto wa miaka sita amefariki dunia akiombewa mlimani alikopelekwa kutolewa mapepo, huku mama yake mzazi akishikiliwa polisi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo akizungumzia tukio hilo amesema lilitokea Februari 18,2018 saa tano asubuhi katika mlima Gambiwe.
Amesema mama wa mtoto Neema Petro (25) na mke mwenzake Raheli Musa (25) walikwenda mlimani na mtoto huyo kwa ajili ya maombi na kufunga
Kamanda amesema wanawake hao wakazi wa kijiji cha Bukulu wilayani Nyang'hwale wanashikiliwa kutokana na kifo cha mtoto Frank Bariki (6), ambaye mwili wake umekutwa na majeraha shingoni na kwenye mbavu.
MTOTO WA MIAKA SITA AFARIKI AKIOMBEWA KUTOA MAPEPO MTOTO WA MIAKA SITA AFARIKI AKIOMBEWA KUTOA MAPEPO Reviewed by KUSAGANEWS on February 21, 2018 Rating: 5

No comments: