Rais Magufuli awasili Uganda

Kampala. Rais John Magufuli leo amewasili nchini Uganda, kuhudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaofanyika  mjini Kampala.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Entebbe, Rais Magufuli amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Sam Kutesa na kisha kuelekea Ikulu ya Entebbe.

Baada ya kuwasili Ikulu amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Uganda  Yoweri  Museveni

Pia kesho atahudhuria mkutano maalum katika ngazi ya wakuu wa nchi unaohusu masuala ya miundombinu na afya na keshokutwa atahudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki




Rais Magufuli awasili Uganda Rais Magufuli awasili Uganda Reviewed by KUSAGANEWS on February 21, 2018 Rating: 5

No comments: