MILIONI 13 ZA SHEREHE ZAELEKEZWA KWENYE MIRADI YA ELIMU NA AFYA


Mbunge mteule wa jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro Dokta Godwin Mollel Amekubaliana na wananchi wake fedha kiasi cha Milioni 13 alizokuwa ametenga kwa ajili ya kufanya sherehe ya kuwashukuru wananchi  kwa kumchagua kuwa mbunge zielekezwe katika miradi ya Elimu na afya.

Baada ya Dokta Mollel Kuchaguliwa katika Februari 17 alifanya ziara kwenye kata tofauti tofauti kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagua wakafanya makubaliano hayo ambapo sasa fedha hizo zinakwenda kutekelezawalichokubaliana na wananchi.

Akizungumza na Kusaga News Mollel amesema kuwa kwasasa jambo lililopo n kuchapa kazi kwasababu porojo zimeisha na wananchi walikuwa wanataka maendeleo ambayo yeye kwa kushirikiana na wananchi wake ameahidi atatekeleza.

“Kweli Ndugu mwandishi baada ya ushindi wa tarehe 17 nilipata nafasi ya kupita kwene kata tano tofauti ,Ngarenairobi,Sanya Juu,Nasai,na kirua na wananchi kwa kweli wananchi tumekubaliana fedha zotehizo za sherehe milioni 13 tuelekeze katika elimu na afya kwa kuwa wao ni wapenda maendeleo namimi ni mbunge wao niliye ahidi kwatumikia”Alisema Mollel
Hata hivyo katika kushurukuru wananchi kwenye kata ya Karansi amechangia wananchi milioni 2 ilikumalizia darasa moja badala y kufanya sherehe.

Mbunge wa jimbo la Siha alichaguliwa tarehe 17 mwezi februari baada ya kurudiwa kwa uchaguzi uliotokana na Mbunge Dokta mollel aliyejiuzulu Chadema na kujiunga na Ccm na kugombea tena na kuchaguliwa na wananchi



MILIONI 13 ZA SHEREHE ZAELEKEZWA KWENYE MIRADI YA ELIMU NA AFYA MILIONI 13 ZA SHEREHE ZAELEKEZWA KWENYE MIRADI YA ELIMU NA AFYA Reviewed by KUSAGANEWS on February 20, 2018 Rating: 5

No comments: