Magufuli " Bodi ya wadhamini UVCCM ivunjwa"


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dk John Pombe Magufuli ametaka kuvunjwa kwa bodi ya wadhamini ya umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM na kuwataka viongozi watakaochaguliwa kuhakiki miradi yote ya umoja huo kuanzia ngazi ya chini.

Akifungua mkutano wa tisa wa jumuia hiyo ambao ajenda yake kuu ni kufanya uchaguzi wa viongozi Rais Magufuli amesema kuwa miradi ya UVCCM mapato yake yamekuwa hayajulikani yanapoenda hivyo inahitaji kuhakikiwa na kuwekwa pamoja ili kuweza kuleta tija kwa umoja huo huku akisema bodi ya wadhamini imekuwa haina msaanda katika jumuia hiyo.
Rais Magufuli pia amewataka UVCCM kuchagua viongozi wanaofaa na wanaoichukia rushwa ili waweze kuisaidia serikali badala ya kuwa viongozi wa kuyumbishwa na misimamo ya watu wenye pesa hali iliyofanya umoja huo kukosa muelekeo hasa kipindi cha uchanguzi

Katika mkutano huo wanachama wapya waliojiunga na chama hicho hivi karibuni kutoka vyama mbalimbali waliwataka vijana wa CCM kuwa mstari wa mbele kuisaidia serikali.
Katika hatua nyingine Rais Magufuli amesema Mwenyekiti wa UVCCM anayemaliza muda wake Sadifa Juma Hamisi anashikiliwa na Tasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa
Magufuli " Bodi ya wadhamini UVCCM ivunjwa" Magufuli " Bodi ya wadhamini UVCCM ivunjwa" Reviewed by KUSAGANEWS on December 10, 2017 Rating: 5

No comments: