Mbunge
wa Bunda Mjini kwa tiketi ya (CHADEMA) Ester Bulaya amekamatwa na jeshi la
Polisi wilayani Tarime na kwenda kufanyiwa mahojiano na polisi Kanda Maalum ya
Tarime na Rorya kwa kile kilichoelezwa kufanya mkutano nje ya jimbo lake.
Akizungumza
Afisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene amesema kuwa mbunge huyo amekamatwa na
jeshi la polisi kwa kushiriki kwenye mkutano wa Mbunge wa jimbo la Tarime
vijijini John Heche uliofanyika jana.
Amesema
Ester amekamatwa na kufikishwa polisi Kanda Maalum ya Tarime na Rorya,na polisi
wamedai kuwa walikuwa wanamtafuta baada ya yeye kushiriki kwenye mkutano wa
hadhara ambao ulifanyika Nyamongo, kwenye jimbo la la Tarime vijijini ambapo
Mbunge John Heche alikuwa na ziara ya jimbo.
Mbunge
Ester Bulaya wiki hii alikuwa na ziara pia katika jimbo lake kusikiliza maoni
mbalimbali ya watu na kuwashukuru wananchi wake kwa kuwa wavumilivu kwa muda
mrefu kufuatia kesi mbalimbali ambazo zilikuwa zikimuandama kutokana na Mbunge
wa zamani wa jimbo hilo kufungua kesi kadhaa mahakamani kupinga ushindi wa
Ester Bulaya
Mbunge Ester Bulaya akamatwa na polisi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 19, 2017
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 19, 2017
Rating:


No comments:
Post a Comment