Watu
wawili wamefariki dunia na wengine 29 wamejeruhiwa baada ya tela la trekta
walilokuwa wamepanda kutoka kitongoji cha Lorngoswani kwenda Kijiji cha Terrat
Wilayani Simanjiro, Manyara kupata ajali na kupinduka
Mkuu
wa wilaya ya Simanjiro Mhandisi Zephania Chaula akizungumza kwa njia ya simu
amesema tukio hilo limetokea leo jumapili saa tatu asubuhi karibu na Kijiji cha
Terrat
Amesema
watu hao walikuwa wakienda kwenye tamasha la kwaya Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri (KKKT) Mhandisi Chaula amesema wanawake wawili walikufa papo hapo
katika ajali hiyo, watu 29 wakiwemo watoto wadogo wawili walikimbizwa hospitali
ya rufaa ya mkoa wa Arusha Mount Meru.
Majeruhi
wenine 15 walitibiwa kwenye zahanati ya Terrat lakin nao baadaye walikimbizwa
Mount Meru baada ya hali zao kuwa mbaya.
Amesema
chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana mara moja ila polisi wameshafika eneo
la tukio kwa uchunguzi zaidi.
Wawili wapoteza maisha ajali ya trekta
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2017
Rating:

No comments:
Post a Comment