Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza kuchukuliwa kwa
hatua kali za kisheria kwa viwanda na migodi inayofanya shughuli zake za
uzalishaji kwa kuharibu mazingira ikiwamo utitirishaji wa kemikali katika
makazi ya watu.
Amesema kufanya hivyo kunahatarisha usalama wa
wananchi na viumbe hai wengine
Mama Suluhu Hassan ametoa agizo hilo Juni 4, kijijini
Butiama mkoani Mara wakati akihutubia wananchi katika kilele cha siku ya
mazingira Duniani
Amesema uharibifu wa mazingira ukiachwa uendee nchini ni
hatari kwa usalama wa maisha na viumbe na hivyo ni muhimu kwa viongozi katika
ngazi zote kuchukua hatua zitakazosaidia kukabiliana na vitendo hivyo
Kutozingatia hifadhi ya mazingira kunaweza kusababisha
kuparaganyika kwa mfumo wa ikolojia na kufanya maisha yetu na ya vizazi
vijavyo kuwa mashakani”. Amesema
Amesema katika kuadhimisha siku ya mazingira Dunia viongozi
wanapaswa kuchukua hatua za kuelimisha wananchi na kuwahamasisha ili kila mtu
ashiriki katika juhudi za kuwa na uchumi unaozingatia hifadhi ya mazingira.
Makamu wa Rais ataka adhabu kali kwa viwanda, migodi inayoharibu mazingira
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 04, 2017
Rating:

No comments:
Post a Comment