Sita wauawa katika shambulio la kigaidi London



Watu sita wameuawa na wengine 48 kujeruhiwa katika shambulio linalodaiwa kuwa la kigaidi leo, jijini London, Uingereza

Polisi nchini humo wamesema, polisi walifanikiwa kuwaua washambuliaji watatu kati yao

Ghasia zilianza baada ya gari moja kuingia ndani ya umati wa watembea miguu, katika daraja kuu jijini London

Taarifa zimesema watu 20 waliojeruhiwa wamepelekwa katika hospitali sita tofauti jijini London

Mwandishi wa BBC Holly Jones, aliyekuwepo katika eneo hilo wakati wa shambulio hilo amesema gari lililohusika lilikuwa linaendeshwa na mwanamume na lilikuwa linaenda kwa kasi

Alilipinda gari karibu nami na akagonga watu watano au sita hivi. Aliwagonga wawili mbele yangu na kisha wengine watatu waliokuwa nyuma yangu," Jones ameiambia BBC.



Sita wauawa katika shambulio la kigaidi London Sita wauawa katika shambulio la kigaidi London   Reviewed by KUSAGANEWS on June 04, 2017 Rating: 5

No comments: