MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNDUA BARABARA YA ST JAMES/KALOLENI ARUSHA

Mkuu wa mkoa wa arusha Bwana Mrisho Gambo amezindua mradi wa barabara yenye urefu wa kilomita 0.65 katika kata ya kaloleni jijini arusha ambapo ni muendelezowa ziara yake ya kikazi ya siku tano kwenye jiji la Arusha.

Akitoa tarifa juu ya mradi huo injinia wa jiji Gaston Pascal kuhusu matengenezo ya barabara ya st James  Kaloleni iliyoinduliwa leo amesema kuwa barabara hiyo imegaramiwa na mfuko wa barabara ambayo imetumia kiasi cha ya shilingi milioni 586.5 mpaka kukamilika na inajumla ya mita 560.

Akizungumza injinia Gaston amesema kuwa lengo la mradi huo ni maboresho ya ya miundombinu ya barabara ndani ya kata ya kaloleni pamoja na wilaya ya Arusha kwa ujumla na uamuzi wa kutengeneza barabara hiyo ulifikiwa kwa ajili ya kupunguza msongamano wa magari katika jiji.

Baada ya kupokea taarifa mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa kutokana na utekelezaji mzuri wa mradi huo serikali itaendelea kuongeza fedha ili kuboresha maendeleo hasa kwa upande wa miundombinu.


Hata hivyo amesema serikali inaendelea kupeleka fedha katika halmashauri zote nchini ikiwemo jiji la Arusha  Arusha kwa kiwango cha lami ambapo ni utekelezaji wa ahadi ya awamu ya tano ya Raisi Dokta John Pombe Magufuli.
MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNDUA BARABARA YA ST JAMES/KALOLENI ARUSHA MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNDUA BARABARA YA ST JAMES/KALOLENI ARUSHA Reviewed by KUSAGANEWS on April 26, 2017 Rating: 5

No comments: