MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZINDUA KITUO CHA POLISI MURIETY


Wananchi wa Kata ya Muriet iliyopo eneo la Kwamrombo Jijini Arusha wataweza kunufaika na ujenzi wa kituo cha Polisi ifikapo Juni mwaka huu mara baada ya kukamilika kwake. 

Wananchi hao ambao juzi walishuhudia uwekaji wa jiwe la msingi uliofanywa na Mkuu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo pamoja na wafadhili wa kampuni ya Lodhia Group ambao wametoa Sh milioni 250  kwaajili ya ujenzi huo unatarajia kukamilika kati ya Juni na Julai mwaka huu. 

Wakitoa neno la shukrani jana eneo la Morombo Jijini hapa wananchi hao ambao ni Rose Msai na Sihaba Said walisema  ujenzi huo utakapokamilika utawezesha  wananchi hao kupata huduma za  usalama wa mali zao ikiwemo ulinzi  kwani Kata hiyo haina kituo cha Polisi na inategemea huduma za ulinzi na usalama kutoka eneo la Mbauda ambapo ni mbali na eneo hilo. 

Masai alisema ujenzi wa kituo hicho utakapokamilika utawezesha wananchi wa Kata hiyo kupata huduma za ulinzi na usalama kwani Kata hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali za usalama kutokana na kukosekana kwa tukio hilo. 

"Tunashukuru kwa ujenzi wa kituo hiki cha polisi na pia tunashukuru kampuni ya Lodhia kwa kutujengea kituo cha polisi ambacho kitahudumia sisi wananchi wa Kata hii kubwa ambayo inachangamoto za kiuhalifu lakini uwepo wa kituo hiki utasaidia wananchi kupata huduma mbalimbali "

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Lodhia Group, Arun Lodhia alisema kampuni yake imetenga faida ya Sh, milioni 200 kwaajili ya wananchi ili kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili hivyo ujenzi wa kituo hicho cha Polisi utawezesha kuzuia uhalifu. 

Alisema ameamua kujenga kituo hicho kwaajili ya kusaidia jamii ya wananchi wa Kata ya Muriet kupata huduma bora za ulinzi na usalama ili kudhibiti matukio ya uhalifu na watajenga nyumba kwaajili ya polisi wanatoa huduma kwa wananchi. 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema kituo hicho kitasaidia wananchi kupata za ulinzi na usalama ikiwemo ujenzi kwa kituo hicho ulioanza mwaka 2016 


Wakati huo huo, Rc Gambo amemwagiza Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Arusha, Mhandisi Gasper Msigwa kuhakikisha wanapeleka nguzo 800 za umeme kwenye maeneo yote ya Kata ya Muriet  pamoja na Terrat na wazisambaze kwenye maeneo hayo kabla ya kupeleka kwingine 
MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZINDUA KITUO CHA POLISI MURIETY MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZINDUA KITUO CHA POLISI MURIETY Reviewed by KUSAGANEWS on April 26, 2017 Rating: 5

No comments: