Askari wa kulinda amani
wa Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya Kati Afrika wanaotokea nchini Tanzania,
ameuawa na waasi huku wengine 18 wakijeruhiwa vibaya.
Kwenye Taarifa iliyotolewa na Jeshi
la Ulinzi Tanzania imesema kwamba kati tukio hilo limetokea Juni 3, 2018 huko
Afrika ya Kati, ambapo kikosi hiko chenye askari 90 kilishambuliwa na waasi
wanaojulikana kwa jina la Sirir, na kusababisha kifo cha askari huyo mmoja,
kujeruhi 18 huku watano kati yao wakiwa katika hali mbaya zaidi.
Majeruhi wa shambulio hilo
wamepelekwa katika Hospitali ya Kanda ya Umoja wa Mataifa iliyopo Bangui
kupatiwa matibabu, huku utaratibu wa kuurejesha mwili wa marehemu nyumbani
Tanzania zikiwa zinaendelea.
Mwanajeshi wa Tanzania auawa, watano hali ni mbaya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 06, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 06, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment