Majambazi yampora Sh39 milioni mfanyabiashara wa ng’ombe

Watu watano wanaosadikiwa ni majambazi, wamevamia nyumba ya mfanyabiashara wa ng’ombe mkoani hapa, Gwaya Ramadhan na kumpora Sh39.8 milioni

Majambazi hayo yakiwa wamefunika sura zao na vitambaa vyeusi huku wakiwa na silaha zinazodaiwa kuwa SMG, walimvamia mfanyabiashara huyo nyumbani kwake mtaa wa Mwayunge, kata ya Igunga Mjini wilayani Igunga Juni 2.

Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Wilbrod Mutafungwa alisema polisi wanaendelea kuyasaka majambazi hayo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano watakapopata taarifa yalipo

Akizungumzia tukio hilo, Ramadhan alisema lilitokea Jumamosi saa 1:00 jioni wakati akifuturu na familia nyumbani kwake

Ramadhan alisema majambazi hayo baada ya kufika nyumbani yaligawanyika sehemu tatu; moja lilibaki getini, jingine lilimteka mmoja wa mtoto wake ili alionyeshe sehemu ya kuzimia taa huku jingine likimuamuru atoe fedha

Alieleza kuwa aliwagomea lakini mmoja wao alitoa amri kwa aliye na bunduki ampige risasi, hali iliyomlazimu kutii kwa kuwaonyesha fedha kwenye gari yake alipokuwa amezihifadhi

Majambazi yampora Sh39 milioni mfanyabiashara wa ng’ombe Majambazi yampora Sh39 milioni mfanyabiashara wa ng’ombe Reviewed by KUSAGANEWS on June 03, 2018 Rating: 5

No comments: