Watu 27 wanashikiliwa mkoani hapa kwa tuhuma
za kuchoma moto kituo kidogo cha Polisi cha Mwandoya katika Wilaya ya Meatu na
kuteketeza samani na mali zote zilizokuwa zikitumiwa na jeshi hilo
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini
kwake jana, Kamishna Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Boniventure Mshongi
alisema tukio hilo lilitokea Machi 22 mwaka huu, saa 2:45 usiku
Kamanda Mshongi alisema wahalifu hao
walivamia kituo hicho wakiwa na matofali, mawe na silaha za jadi na kuharibu
samani zote na kisha kuchoma moto nyaraka mbalimbali za kituo hicho.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mali nyingine
zilizoharibiwa kwa kuchomwa moto na majambazi hayo ni milango sita, meza tatu,
viti vitano vya mbao na vingine 16 vya plastiki na kabati la kutunzia mafaili
ya kituo
Vingine vilivyoharibiwa ni mashine ya
kupimia kilevi na pikipiki yenye namba DFPA 1171 mali ya polisi
“Baada ya kutekeleza uhalifu huo, kundi hilo
lilikwenda kwenye makazi na vibanda vya biashara vya askari polisi wanaofanya
kazi kituoni hapo pamoja na duka la kuuza dawa za binadamu la Magreth Isapi
wakafanya uhalifu pia kwa kuchoma moto mali hizo,” alisema
Aliongeza, “Walikwenda pia nyumbani kwa
askari ambaye anaishi uraiani kitongoji cha Muungano na walichoma moto nyumbaaliyokuwa akiishi na kuunguza vitu vyake vyote pamoja na vyeti vya taaluma ikiwamo vyeti vya sekondari, udereva na walichoma pia cheti cha ndoa na
kompyuta ya askari huyo
Alisema kuwa watuhumiwa hao walichoma maduka
yanayomilikiwa na askari kisha kuiba kompyuta, kamera na vifaa vingine
vinavyotumika kusafishia picha
Kamanda Mshongi alisema kundi hilo pia lilikwenda kwenye duka la dawa la Magreth Isapi na kuvunja mlango na kuiba dawa mbalimbali za binadamu ambazo thamani yake haijajulikana na baadaye kulichoma moto
‘’Wakati kundi hilo likiendelea na uharibifu
kuelekea maeneo mengine, polisi Meatu wakiongozwa na OCD F. Bongole akisaidiwa na
Kaimu OC/CID Nassib waliwahi eneo la tukio na kuwadhibiti wahalifu hao, na hadi
sasa thamani ya vitu vilivyoharibiwa na kuibiwa bado haijafahamika’’ alisema
Kamanda Mshongi
Katika tukio linalofanana na hili mwaka
2015, kundi la watu zaidi ya 100 wakiwa na silaha mbalimbali za jadi walivamia
kituo kidogo cha polisi cha Mbingu, wilayani Kilombero mkoani Morogoro na
kukichoma moto, wakishinikiza kukabidhiwa mtuhumiwa aliyedaiwa kumuua mkewe ili
wamuue
Tukio hilo lililothibitishwa na Kamanda wa
Polisi wakati huo, Leonard Paulo, lilijiri saa chache baada ya mtuhumiwa
Bashiri Ernest Kadugula kufikishwa kituoni hapo akikabiliwa na tuhuma za kumuua
mkewe,Veronica Chambula kwa kumkatakata kwa panga baada ya kutokea tofauti baina
yao.
Watu 27 wakamatwa kwa madai ya kuchoma kituo cha polisi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 24, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment