Mwenyekiti wa Umoja wa
Vijana wa Taifa UVCCM, Kheri James amewataka vijana wa umoja huo kuwa tayari
kulinda heshima ya nchi kwa gharama yeyote dhidi ya vibaraka ambao wanataka
kuchafua taswira ya nchi kwa lengo la kuwanufaisha mabeberu.
Kheri ametoa kauli hiyo wakati
akizungumza na vijana wa umoja huo mjini Dodoma na kusema lengo la kufanya
hivyo ni kutokana na kuwepo na matumaini makubwa ya kiuchumi yaliyorejeshwa na
serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli hivyo hawapo
tayari kuona kikundi cha watu wachache wanaotaka kuwarudisha nyuma kimaendeleo.
"kuanzia sasa endapo akiibuka
mtu mwenye ujasiri wa kutukana, vijana hawatotukana bali watafanya
litakaloonekana linafaa kwa maslahi ya taifa kwani wapo wanaojipambanua wazi
kusifu viongozi wa ulimwengu mzima lakini kamwe hawawezi kuwapongeza na kuwasifu
kwa chochote viongozi wa nchi", amesema Kheri James.
Naye Kaimu Katibu UVCCM, Shaka Hamdu
Shaka amesema serikali imeona uwepo wa vijana makao makuu na kuthamani uwepo
wao kutokana na kuendesha mambo kisasa zaidi.
Kwa upande wake mbunge wa viti
maalum vijana, Mariam Mzuzuri amesema maamuzi na tamko la mwenyekiti wa uvccm
taifa watalifanyia kazi ili vijana waweze kutambua fursa walizonazo hususania
mkoani Dodoma ambako hivi sasa ni makao makuu ya nchi.
UVCCM wasema watalinda nchi kwa Gharama Yeyote
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 26, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment