Aliyekuwa diwani wa Kata ya Olsunyai mkoani Arusha, Elirehema Nnko kwa tiketi ya (CHADEMA) ambaye amekihama chama chake na kujiunga CCM amefunguka na kusema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaangalia watu wa kuwachukua kutoka upinzani.
Elirehema Nnko
amesema hayo alipokuwa akihojiwa na moja ya chombo cha habari na kusema kuwa
yeye amechukuliwa na CCM kwa kuwa anajiweza na kudai ili uchukuliwe na CCM basi
lazima uwe jembe kwani kitu kizuri
kinajiuza.
"Sikiliza
nikwambie CCM wenyewe wanaangalia mtu wa kumchukua hawachukui tu kila mtu
lazima kidogo uwe unajiweza yaani uwe jembe na unaweza kupiga kazi wewe
unafikiri kuna mtu anachukua mazaga zaga, mimi najua kizuri
kinajiuza pia"
Mbali na hilo Diwani
huyo ameelezea kuhusu baadhi ya picha zake zenye utata na kusema kuwa watu
ambao wanamzungumzia vibaya kuhusu mapozi yake hayo ni wana wivu na yeye hakuna
lingine ila yeye amechukulia hilo kama ni mtu ambaye ana nguvu ndiyo maaana
watu wanamzungumzia sana.
Viongozi wengi wa
upinzani wanapohama kutoka vyama vyao na kwenda CCM wamekuwa wakisema kuwa
wanavutiwa na utendaji kazi wa serikali ya awamu ya tano, wengine wakisema
wanavutiwa na kasi ya Rais lakini huyu amedai ameenda kwaajili ya biashara
zake.
NIMECHUKULIWA NA CCM KWASABABU NAJIWEZA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 15, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 15, 2018
Rating:



No comments:
Post a Comment