Mwakyembe apongeza hatua ya Baraza la Habari Tanzania, MCT, ya kufungua kesi katika Mahakama ya Afrika mashariki
Waziri
wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harison Mwakyembe amepongeza hatua
ya Baraza la Habari Tanzania, MCT, ya kufungua kesi katika Mahakama ya Afrika
mashariki kupinga Sheria mpya ya Huduma za Habari ya mwaka 2016.
Dk. Mwakyembe
amesema, Tanzania ni miongoni mwa nchi 6 Barani Afrika zilizoridhia mkataba wa
kuruhusu wananchi wake kuishtaki serikali katika Mahakama ya Kimataifa, na
kwamba hatua hiyo inaonesha namna ambavyo wananchi wameanza kutambua namna bora
ya kuwasilisha malalamiko yao.
Hivi karibuni Baraza
la Habari Tanzania MCT, lilifungua kesi dhidi ya serikali kupinga Sheria mpya
ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 kwa madai kuwa inanyima uhuru wa vyombo vya
habari.
Awali kabla ya tamko
hilo, Dkt Mwakyembe amekutana na mabalozi wa nchi za Marekani na China kujadili
namna ya kuhifadhi na kuendesha programu ya kumbukumbu za ukombozi wa bara la
Afrika ambayo Tanzania imepewa na nchi za Afrika, kutokana na kuwa kinara
katika kusimamia mapambano dhidi ya wakoloni na uhuru wa nchi za Afrika
Mwakyembe apongeza hatua ya Baraza la Habari Tanzania, MCT, ya kufungua kesi katika Mahakama ya Afrika mashariki
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 15, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 15, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment