Madiwani 2 kupitia chama cha demokrasia na maendeleo
CHADEMA katika halmashauri ya jiji la Arusha wamejivua nafasi zao za udiwani na
kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha mapinduzi Ccm kwa kile walichodai
kuwa ni kumuunga mkono raisi magufuli kwa utendajinkazi wake mzuri wa kazi ya
kutumikia wananchi.
Madiwani hao ambao ni diwani wa kata ya Daraja mbili
Bwana Prosper Msofe na diwani wa kata ya Terati Bwana Obedi Mosses Meng’oriki
wamesema kuwa wameamua kujiunga na chama cha mapinduzi kwa kuwa huko walikokuwa
wanaishi kwa migogoro.
Wamesema kuwa chama cha Demokrasia na maendeleo kimekuwa
kama chama cha mtu flani ambapo wanakosa uhuru wa kuwatumikia wananchi hivyo
wakaona wamuunge mkono raisi kwa kazi anayofanya.
Bwana Msofe amesema kuwa kwa jiji la Arusha chadema
kimekuwa chama cha mbunge Godbless Lema jambo ambalo haliwezi kuwaletea
wananchi maendeleo huku meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro akikataa
kukosolewa kutokana na uwezo wake mdogo wa kuongozahalmashauri hiyo ya jiji la
Arusha.
Mpaka sasa kata ambazo madiwani wake wamejiunga na CCM
ni kata ya Murieti (Credo Kifukwe) Kata ya Kimandolu(Rayson Ngowi)Kata ya
daraja mbili (Prosper Msofe)Kata ya Terati (Obedi Mosses Meng”oriki)
MADIWANI WA CHADEMA ARUSHA WAHAMIA CCM
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 20, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment