Kenya: Mwanasheria mkuu amkosoa Raila kwa kutaka kujiapisha


Hatua ya kiongozi wa upinzani nchini Kenya ya kujiapisha imepata pigo baada ya mwanasheria mkuu Githu Muigai kusema kuwa hatua hiyo ni uhaini na hukumu yake ni kifungo cha maisha jela.

Hatua ya kiongozi wa upinzani nchini Kenya ya kujiapisha imepata pigo baada ya mwanasheria mkuu Githu Muigai kusema kuwa hatua hiyo ni uhaini na hukumu yake ni kifungo cha maisha.

Akizungumza  na wanahabari Muigai  amesema hatua ya mabunge ya majimbo kupitisha miswada ya kuanzisha vikao vya mabunge ya wananchi pia ni kinyume cha sheria.

Aidha marekani imemtaka Odinga kutojiapisha ikisema ni ukiukwaji wa sheria. Wakati huo huo Odinga ameilani vikali jamii ya kimataifa kwa kunyamazia ukiukaji wa haki za binadamu baada ya uchaguzi mkuu uliotekelezwa na maafisa wa polisi. 

Tamko la mwanasheria mkuu Githu Muigai linajiri siku nne kabla ya kiongozi wa upinzani raila Odinga kujiapisha kwa kutumia mabunge ya majimbo.


Tayari majimbo 12 yamepitisha mswada wa kujenga vikao vya mabunge ya wananchi ambayo hayatambui uhalali wa rais Kenyatta. Kama ishara ambayo serikali ya rais Uhuru Kenyatta haitavumilia hatua ya Odinga, Muigai alisema.
Kenya: Mwanasheria mkuu amkosoa Raila kwa kutaka kujiapisha Kenya: Mwanasheria mkuu amkosoa Raila kwa kutaka kujiapisha Reviewed by KUSAGANEWS on December 09, 2017 Rating: 5

No comments: