CHADEMA yampongeza Raisi Magufuli kwa kufanya kitendo cha ajasiri

 
 Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, kimechukua hatua ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kitendo cha kuwasamehe wafungwa wakiwemo Babu Seya na mwane Papii Kocha.

Kwenye Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, chama hiko kimesema ni kitendo cha ujasiri kwa Rais Magufuli kuendelea kutekeleza ahadi ambazo zilitolewa na chama hiko wakati wa kampeni zake mwaka 2015.

Sambamba na pongezi hizo, CHADEMA pia kimeomba serikali kutumia mamlaka iliyonayo kufuta kesi za mashehe wa Zanzibar ambao kesi yao iko mahakamani, pamoja na watu mbali mbali wenye kesi za makosa ya kimtandao.


Isome hapa taarifa yote 
CHADEMA yampongeza Raisi Magufuli kwa kufanya kitendo cha ajasiri CHADEMA yampongeza  Raisi Magufuli kwa kufanya kitendo cha ajasiri Reviewed by KUSAGANEWS on December 09, 2017 Rating: 5

No comments: