KIWANDA CHA KUTENGENEZA MAGUNIA YA KATANI MOROGORO CHAFUNGWA KWA KUKOSA SOKO



Kiwanda cha kutengeneza magunia ya katani kilichoanza uzalishaji wake mwaka 1998 mkoani Morogoro (TPCM) kimefungwa na kusitisha uzalishaji tangu April 2016 kufuatia kukosa soko la bidhaa hiyo hatua ambayo imetajwa kusababishwa na uingizwaji wa mifuko ya viroba kutoka nje ya nchi huku ajira za wafanyakazi 900 wa kiwanda hicho zikisitishwa.

Kufungwa kwa kiwanda hicho kumebainika wakati wa ziara ya Mkuu wa mkoa huo Kebwe Steven Kebwe ya kukagua hatua walizofikia wamiliki wa viwanda katika kufufua na kuanza uzalishaji

Katika hatua nyingine kilichokuwa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kula yanayotokana na mbegu za alizeti cha Moprock kimeanza uzalishaji baada ya kusitisha uzalishaji huo kwa zaidi ya miaka minane iliyopita,huku kikitarajia kumaliza tatizo la ukosefu wa soko la alizeti kwa wakulima wa mikoa ya Morogoro,Dodoma pamoja na Singida

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dokta Kebwe amemuagiza Mkurugenzi wa Moprock kumalizia ukarabati uliobaki ili uzalishaji uendelee huku akieleza kusikitishwa na hatua ya kiwanda cha magunia kusitisha uzalishaji
KIWANDA CHA KUTENGENEZA MAGUNIA YA KATANI MOROGORO CHAFUNGWA KWA KUKOSA SOKO KIWANDA CHA KUTENGENEZA MAGUNIA YA KATANI MOROGORO CHAFUNGWA KWA KUKOSA SOKO Reviewed by KUSAGANEWS on July 09, 2017 Rating: 5

No comments: