Samia awawashia moto waajiri



Makamu wa Rais, Samia Suluhu amewaagiza waajira wasiopeleka au kuchelewesha michango ya wanachama kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii nchini wachukuliwe hatua za kisheria ili kukomesha tabia hiyo

Samia ametoa kauli hiyo leo Jumamosi jijini Mwanza wakati anafungua semina ya maisha baada ya kustaafu,fursa ya mafao, uwekezaji iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) kwa ajili ya wastaafu watarajiwa 450 kutoka wilaya zote za Mkoa wa Mwanza.

Amesisitiza kuwa waajiri wakichangia kwa mujibu wa sheria kwenye mifuko hiyo watawezesha wanachama wao kupata mafao kikamilifu na kwa wakati.

Kuhusu madeni ya Serikali kwa mifuko ya hifadhi ya jamii nchini, Samia amewahakikishia wakurugenzi wa mifuko hiyo kuwa Serikali inashughulikia madeni hayo na baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki wa madeni basi malipo yatafanyika haraka iwezekanavyo.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha michango ya pensheni kwa wafanyakazi wa taasisi zinazopata ruzuku kutoka serikalini inalipwa kwenye mifuko hiyo kwa wakati.

Samia awawashia moto waajiri Samia awawashia moto waajiri Reviewed by KUSAGANEWS on June 03, 2017 Rating: 5

No comments: