MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA ATHUMANI KIHAMIA AMALIZA MGOGORO WA WAFANYABISHARA ULIOFURUKUTA KWA MUDA MREFU
![]() |
Mkurugenzi wa jiji la Arusha akizungumza na wafanyabiashara |

Akizungumza na wafanyabiashara hao
wa pande zote mbili kihamia Amesema kuwa mgogoro huo umeisha na makubaliano ni kwamba
baina ya vikao vya madiwani ni kuwa wajenzi hawajamalizana na halmashauri hivyo
wataendelea kumiliki vibanda hivyo mpaka hapo maelekezo mengine yatakapotolewa.
”””Katika kuona tuwasaidieje
nimeongea na pande zote mbili kwa vipindi tofauti kuna makubaliano maalum
ambayo tumekubaliana kila upande lakini na kuyaleta pamoja na kwasasa hivi
nayatangaza kama ifuatavyo mbele yao kubaliano namba moja ni namna ambavyo kodi
italipwa kwamba kwa kuwa wajenzi wamejenga vibanda na jiji hawajamalizana nao
mana ake ni wazi kwamba wanamiliki bado vibanda na tumekubaliana tuwape
mikataba ya muda mrefu hii ni kwa mujibu wa kikao cha kamati ya madfiwani”””
Kihamia amesema hayo yamekuja baada
ya vikao mbalimbali vya baraza,pamoja na vikao vya kamati ya fedha
vinavyohusisha madiwani na makubaliano yao ni kuwa mfanyabiashara ambaye ni
mpangaji atalipa kodi kwa mfanyabiashara mjenzi na mjenzi atalipa halmashauri
kwa mujibu wa mkataba ambao wameingia ili kutatua jambo hilo na lifikie mwisho.
Pia amesema kuwa yeye kama mkurugenzi kwa muda mrefu amewashawishi wafanyabiashara
mpaka wametoa kesi iliyokuwepo mahakamani lengo ni ili kuona watakavyo maliza
mgogoro huo na sasa amewashukuru kwa kukubaliana ili kuendelea kujenga jiji la
Arusha.
Akizungumza kwa niaba ya
wafanyabiashara wapangaji Josephine Esuphat wamemshukuru mkurugenzi Kihamia kwa
kuwa suala hilo huenda lingeleta matatizo baina yao na wamepata moyo na
serikali ya awamu ya tano kwa kuwajali wafanyabiashara hao.
Naye mwenyekiti wa jumuiya ya
wafanyabiashara Bwana Lokeni Adolf Masawe amesema amemshukuru mkurugenzi kwa
kujali pande zote mbili ambazo zilikuwa na mgogor.
MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA ATHUMANI KIHAMIA AMALIZA MGOGORO WA WAFANYABISHARA ULIOFURUKUTA KWA MUDA MREFU
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 03, 2017
Rating:

No comments:
Post a Comment