RC ANYWA MAJI MBELE YA WANANCHI KUWAHAKIKISHIA KWAMBA HAYANA MADHARA KIAFYA



Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo pamoja na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jiji la Arusha (AUWSA) Injinia Ruth Koya wamealazimika kunywa maji mbele ya wananchi wa Kata ya Olasiti wanayidai kuwa yanachumvi nyingi na hayafai kwa matumizi ya binadamu. 

Gambo alilazimika kunywa maji hayo mara baada ya wananchi kulalamika kuwa maji hayo ya Auwsa si salama kwa afya zao na yanachumvi kupita kiasi hali inayosababisha usalama wa afya zao kuwa mashakani. 

Wakitoa malalamiko yao Jijini hapa, mmoja kati ya wananchi hao Hawa Ismail amesema maji yanatokana kwa nadra na eneo wanalochotea maji hayo ni mbali hali inayopelekea baadhi yao kununua maji safi mjini au kwenye magari maalum kama boza kwa kuchanhishana Sh, 70000 ili waweze kunywa maji mazuri. 

Ili kuonyesha kama maji haya ni salama ngoja ninywe mimi na Mkuu mbele yenu halafu tuone kama tutapata madhara au la lakini niwahakikishie kuwa maji haya hayana madhara yoyote kwa wananchi. 

Awali Mkurugenzi wa Auwsa, Mhandisi Ruth Koya alisema maji hayo hayanachumvi kubwa kama wanavyodai wananchi hao na yamepimwa na wataalam wa maji ni salama kwa matumizi ya binadamu hivyo waendelee kuyatumia ili wakati wakitafuta wataalam wa kuwasaidia kudhibiti chumvi hiyo. 

Awali kabla ya Rc Gambo kuzindua ujenzi wa tenki la Maji Mlima Burka  Koya alisema  mradi huo wa maji kutoka kisima cha Magereza  umesaidia uboreshaji wa maji katika Kata mbalimbali ikiwemo Kata hiyo. 

Amesema gharama za ujenzi wa tanki hilo ni Sh, milioni 135,020,960 hadi kukamilika kwake na utasaidia kutatua kero ya maji kwenye Kata ya Muriet na Terrat ifikapo Julai mwaka huu

Pia Gambo amepongeza mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira AUWASA kwa kufanya kazi nzuri ya kutatua kero ya maji kwenye baadhi ya maeneo ya jiji la Arusha.

Gambo amesema kuwa yeye kama kiongozi mkuu wa serikali ya mkoa atahakikisha anawapa nguvu watumishi wa serikali ili kuendelea ili kuboresha huduma mbalimbali ambazo zimekuwa zikikabili wananchi wa hali ya chini.


Pia Rc Gambo alitoa rai kwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia kutenga fedha kwaajili ya kulipa deni la walimu waliosimamia mitihani wa darasa la nne kw shule za msingi badala ya kusubiri fedha kutoka hazina na pindi zitakapokuja fedha hizo zitarejeshwa kwenye kifungu kilichokopwa fedha hizo ili kuondoa manung'uniko ya walimu wanaodai malipo ya mitihani pamoja na fedha za nauli.

Aidha Gambo amemwagiza Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia kuhakikisha anatenga fedha za kuwalipa walimu waliosimamia mitihani wa darasa la nne mwaka jana ambao wanadai jumla ya Sh, milioni 52.

RC ANYWA MAJI MBELE YA WANANCHI KUWAHAKIKISHIA KWAMBA HAYANA MADHARA KIAFYA  RC ANYWA MAJI MBELE YA WANANCHI KUWAHAKIKISHIA KWAMBA HAYANA MADHARA KIAFYA Reviewed by KUSAGANEWS on April 27, 2017 Rating: 5

No comments: