MKUU WA MKOA WA ARUSHA MRISHO GAMBO AAGIZA KURUDISHWA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA JIJI LA JUMA IDI KUJA KUJIBU TUHUMA ZINAZOMKABILI
Mkuu wa mkoa
wa Arusha Bwana Mrisho Gambo amemuagiza katibu tawala mkoa Richard Kuitega kuandika
barua Kwenda Tamisemi ya Kuwasimamishwa kazi watumishi watatu wa halmashauri
akiwemo aliyekuwa mkurugenzi wa jiji la Arusha Bwana Juma Iddi.
Akizungumza
katika mkutano wa watumishi,wazee,vikundi vya akina wanawake, vijana,
madiwani,watendaji wa kata ,viongozi wa dini na wakimila,katika ziara yake ya
siku tano aliyoianza mkoani Hapa kwa ajili ya kuzungumza na wazee,kuzindua
miradi,pamoja na kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo.
Gambo amesema
kuwa watumishi hao ni Bakari Salum Aliyekuwa
Mganga wa Jiji la Arusha ,aliyekuwa mweka Hazina Kessy na Mkurugenzi Juma Idd kwa
kukiuka sheria ya manunuzi ya umma.
Moja kati ya
tuhuma hizo ni matumizi ya fedha ya posho ya ukaguzi kwa shilingi milioni 64.7,ambazo walijilipa
watumishi watumishi zaidi ya 2O.
Aidha gambo
amewataja watumishi hao kuwa ni Allen Sumari,Amani lyimo,Anjela mhetu,babila
Shilogela,Baraka Ahmad,Cloudia Kkidunda,Cleti Sadala,Dickson Laizer,Dkt.Bakari
Salum,Dikson lazier,dkt,Baraka Munde,dkt,Yunus Minja,dkt,Isri Ismail,dkt.Japhet
Kiuvuyo,Dkt.Josiah Mlay,dkt,Thomas Kway,Dkt.Elly Mrema,Farida Minja,fausta
kambaga,Goodluck Ekwabi,hamida kaligaliga,happy saigurani,Hassan abdallah
,james lobikoki,Jane Baralukuliliza, na Joel Msuya.
Amesema huko
nyuma kumekuwa na utaratibu wa kutumia fedha za umma kama shamba la bibi na
kunufaisha watu wachcahe na sio kunufaisha wananchi wengi hivyo watakaobanika
kukiuka taratibu basi na kuvunja sheria hatua kali za kisheria zitachukuliwa
dhidi yake.
MKUU WA MKOA WA ARUSHA MRISHO GAMBO AAGIZA KURUDISHWA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA JIJI LA JUMA IDI KUJA KUJIBU TUHUMA ZINAZOMKABILI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 25, 2017
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 25, 2017
Rating:


No comments:
Post a Comment