ALIEKUWA MWENYEKITI WA UVCCM ARUSHA AACHIWA HURU.



Mahakama ya hakimu mkazi arusha imetoa hukumu ndogo ya kesi ya aliekuwa mwenyekiti wa umoja wa vijana wa ccm arusha (UVCCM) Lengai Ole Sabaya  na kumuachi  huru mshitakiwa baada ya jamuhuri kushindwa kukamilisha ushahidi  zaid wa kesi hiyo.

Akitoa hukumu hiyo ndogo hakimu mkazi Gwantwa Mwankuga amesema kuwa awali kesi hiyo namba 376 ya mwaka 2016 ilifutwa na mahakama ikashuhudia mshitakiwa huyo akikamatwa tena katika eneo la mahakama na kufunguliwa kesi namba 493 mwaka jana.

Kufuatia tukio hilo mahakama inajiuliza ni kipi kilichopelekea kukamatwa tena kwa mshitakiwa ambapo awali jamuhuri ilitakiwa kuleta mashahidi wa kesi hiyo suala ambalo kwa upande wa muendesha mashitaka hilo kuweza kufanikishwa ambapo jamuhuri imeeleza kuwa mashahidi wao wa muhimu juu ya kesi hiyo mmoja yupo nchini kenya na mwengine yupo nje nchi.

Hakimu Gwantwa ameeleza kuwa baada ya kupitia shitaka hilo na hoja za pande zote mahakama imekataa ombi ya mwendesha mashitaka hivyo imeamua  kumuachia huru chini ya kifungu namba cha sheria namba 225/5.

Lengai Ole Sabaya ambae pia ni diwani wa kata ya sambasha wilayani arumeru alifikishwa mahakamani mwaka jana  kwa tuhuma za kugushi vitambulisho vya usalama wa taifa.




ALIEKUWA MWENYEKITI WA UVCCM ARUSHA AACHIWA HURU.  ALIEKUWA MWENYEKITI WA UVCCM ARUSHA AACHIWA HURU. Reviewed by KUSAGANEWS on April 28, 2017 Rating: 5

No comments: