Bingwa wa rekodi ya dunia katika
mbio za mita 800 Dunia mkenya David Rudisha ameshindwa tena kwa mara
nyengine katika mbio hizo na Bingwa katika mbio hizo Nijel Amos wa
Botswana.
Rudisha tayari alikuwa ameongoza mbio hizo akiwa mbele
na ilikuwa imesalia mita 300 kufika katika utepe,wakati Nijel Amos
alipotoka nyuma na kumshinda.Rudisha wakati huohuo mwanariadha wa
Marekani Justin Gatlin aliweka mda bora wa pili mwaka 2015 baada ya
kumshinda Asafa Powel na Tyson Gay katika mbio za mita 100 katika mbio
za Diamond League mjini Lausanne
Mwanariadha huyo mwenye umri wa
miaka 33 ambaye amehudumia mara mbili marufuku ya kutumia dawa za
kusisimua misuli alikimbia mda wa sekunde 9.75 kabla ya mashindano ya
mwezi ujao ya dunia.
Powell na Gay wote wamekimbia mda wa sekunde
9.92 huku Usain Bolt akiwa bado anauguza jeraha,ijapokuwa ana mpango wa
kutetea taji lake katika mbio za Olimpiki mjini Beijing.
RudishaTyson Gay na Jamaica Powell pia walihudumia marufuku ya kutumia dawa za kusisimua misuli.Gay
mwenye umri wa miaka 32 alihudumia marufuku ya mwaka mmoja baada ya
kupatikana ametumia dawa hizo aina ya anabolic steroid mwaka 2013,huku
Powell akihudumia marufuku ya miezi sita baada ya kupatikana ametumia
dawa hizo mwaka 2013.
Nijel Amos amshinda tena Rudisha
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 10, 2015
Rating: 5
No comments:
Post a Comment