Kiwango cha unyanyasaji wa wanahabari duniani chaongezeka

Matukio ya utekaji wanahabari, kuibuka kundi la watu wasiojulikana, kufungiwa vyombo vya habari na kupigwa faini kwa vyombo hivyo vimetajwa kudunisha  uhuru wa habari nchini

Wakisoma hotuba zao leo Mei 3  katika  maadhimisho ya Siku  ya Uhuru wa Vyombo vya habari,  Mwenyekiti wa Vyombo vya habari kusini mwa  Afrika, tawi la Tanzania, (Misa- Tan) Salome Kitomari amesema ni muhimu hatua zichukuliwe kukabiliana na hali iliyopo sasa

Kitomari amesema, takwimu za  taasisi kama waandishi wasio na mipaka na kamati ya kulinda  waandishi wa habari zinaonesha kushuka  viwango vya uhuru wa habari na kujieleza Tanzania

"Lakini pia matukio ya utekwaji nyara na viwango vya unyanyasaji wa wanahabari duniani vimeongezeka sana"amesema

Amesema mwaka jana zimeripotiwa kesi za kupotea kwa waandishi wa habari, manyanyaso na ukiukwaji wa uhuru wa vyombo vya habari

“Leo ni siku ya 163 tangu kupotea kwa mwandishi wa habari wa Mwananchi, hakuna hata fununu tu yupo wapi ama yupo hao ni jambo ambalo linatia doa nchi yetu,"amesema

Amesema wahabari wanaitaka Serikali kupitia jeshi la polisi kuwatafuta waliohusika na kitendo hicho na kuwachukulia hatua za kisheria

Kaimu Mwenyekiti wa  Jukwaa la Wahariri, (TEF) Deodatus  Balile amesema mazingira ya kazi ya kuandika habari yamekuwa magumu kutokana na  baadhi ya watendaji wa vyombo vya dola kubugudhi na kuwafanyia uonevu wanahabari, huku kukiibuka kundi la watu wasiojulikana


Kiwango cha unyanyasaji wa wanahabari duniani chaongezeka Kiwango cha unyanyasaji wa wanahabari duniani chaongezeka Reviewed by KUSAGANEWS on May 03, 2018 Rating: 5

No comments: