Viongozi Mtwara watakiwa kufuatilia watu wanaotaka kuharibu masoko ya korosh


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa mkoa wa Mtwara kupambana na makundi ya watu yanayotaka kuharibu masoko ya korosho.
Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa mnunuzi aliyekataa kununua korosho kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha ubora wa korosho alichokikuta ghalani.
Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba.
“Tandahimba korosho zote ni daraja la kwanza sasa korosho chafu zinatoka wapi? Kuna kundi linataka kuharibu soko lazima tupambane nalo.”
Waziri Mkuu ameongeza kuwa  “lazima mshirikiane kuwabaini walioleta korosho chafu Tandahimba na wakipatikana wachukuliwe hatua kali za kisheria.”
Amesema haiwezekani mnunuzi amenunua korosho daraja la kwanza alafu anakuja anakuta korosho nyingine tena chafu, lazima waliozibadilisha wasakwe.
Awali, Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kubangua korosho cha Amama Farms, ambapo ametoa wito kwa walionunua viwanda vya korosho wafunge mashine mpya na kuanza uzalishaji.
Hata hivyo amewataka wamiliki wa viwanda vyote vya kubangulia korosho washirikiane na Serikali katika kufuata utaratibu wa kununua korosho.
Pia Waziri Mkuu amezindua barabara yenye urefu kilomita tatu iliyojengwa kwa kiwango cha lami ambayo imegharimu sh. bilioni 1.38 zilizotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba.
Kwa upande wake Meneja wa Kiwanda hicho Kwa Mahmoud Sinani alisema korosho zinazobanguliwa kiwandani hapo zinauzwa ndani na nje ya nchi.

Amesema katika awamu ya kwanza ya uwekezaji huo umegharimu sh. bilioni 12 na wanatarajia kuendelea na awamu ya pili ambapo watawekeza dola milioni 20.
Amesema kwa sasa kiwanda hicho kimeajiri watumishi 250 na wanatarajia kuajiri watumishi 1,500 mara baada ya kumaliza awamu ya pili ya upanuzi wa kiwanda.
Pia Waziri Mkuu amewapongeza watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba kwa kuweka kipaumbele katika ujenzi wa miundombini ya barabara kwa kiwango cha lami.

Viongozi Mtwara watakiwa kufuatilia watu wanaotaka kuharibu masoko ya korosh Viongozi Mtwara watakiwa kufuatilia watu wanaotaka kuharibu masoko ya korosh Reviewed by KUSAGANEWS on March 21, 2018 Rating: 5

No comments: