MADEREVA 64 WA ARUSHA ,MANYARA,NA KILIMANJARO WAFUNGIWA LESENI KWA UZEMBE WA KUTOFUATA SHERIA ZA BARABARANI
Jeshi la
polisi kikosi cha usalama barabarani limewakamata madereva 64 wa mabasi ya abiria na kuwaweka rumande na
kuzifungia kwa miezi 6 leseni zao katika mikoa ya arusha,manyara ,na Kilimanjaro
waliokutwa na makosa mbalimbali ikiwemo kosa la mwendokasi katika oparesheni
maalum ya jeshi hilo .
Kamanda wa
kikosi cha usalama barabarani nchni Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Fortunatus
Musilimu amesema oparesheni hiyo imetokana na mikoa ya kanda ya kaskazini kuwa
miongoni mwa mikoa yenye ongezeko kubwa la ajali za barabarani hivyo wameamua
kukomesha tabia hiyo na madereva wote waliokamatwa watafikishwa mahakamani.
Bonyeza hapo chini umtazame kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini akizungumza kuhusu kufungia madereva hao.
MADEREVA 64 WA ARUSHA ,MANYARA,NA KILIMANJARO WAFUNGIWA LESENI KWA UZEMBE WA KUTOFUATA SHERIA ZA BARABARANI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 10, 2017
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 10, 2017
Rating:


No comments:
Post a Comment