CHADEMA kupeperusha bendera nusu mlingoti



Kufuatia kifo cha mmoja wa Waasisi wa CHADEMA, Mzee Philemon Ndesamburo Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Dkt. Vincent Mashinji, ametoa maelekezo kwa watendaji nchi nzima kupeperusha bendera nusu mlingoti.

Mashinji ametoa maelekezo hayo leo wakati akiongea na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam na kusema bendera zinapaswa kupeperushwa nusu mlingoti hadi mwili wa kiongozi huyo utakapopumzishwa katika nyumba yake ya milele. 

Amesema Chama kitashiriki katika msiba huo kwa heshima zote ili kumuenzi mmoja wa waasisi wa siasa za mabadiliko ya kweli na Uhuru wa kweli nchini.

Amesema kuwa msiba huo ni msiba wa CHADEMA, ni msiba wa Watanzania, ni msiba wa Taifa lote kutokana na mchango mkubwa wa Mzee ndesamburo  kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa nchi ya Tanazania na ndiye aliyekifadhili Chama kwa mara ya kwanza kwa kukipatia ofisi eneo la Kisutu jijini Dar es salaam.
CHADEMA kupeperusha bendera nusu mlingoti CHADEMA kupeperusha bendera nusu mlingoti Reviewed by KUSAGANEWS on June 01, 2017 Rating: 5

No comments: