Wanafunzi waliomaliza Elimu ya Msingi Ruvuma hawajui Kusoma


Wadau wa elimu mkoani Ruvuma wamesikitikitishwa na kiwango kikubwa cha wanafunzi kumaliza elimu ya msingi wakiwa hawajui kusoma na kuandika hali inayosababisha kuzalisha wasomi walio na uwezo mdogo hivyo wametoa mapendkezo ya kukomesha hali hiyo.

Wakizungumza katika Maadhimisho ya wiki ya Elimu mkoani Ruvuma wamesema kuwa kunatakiwa mabadiliko makubwa ya mitihani ili kuweza kuzalisha wanafunzi wenye uwezo kuliko mitihani ya sasa ya kuchagua ambayo inamfanya mwanafunzi kufaulu elimu ya msingi akiwa hajui kusoma na kuandika.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa mkoa wa Ruvuma Bw.Ephraim Simbeye anasema kuwa mkoa wa Ruvuma unafafanya jitihada kupunguza idadi kubwa ya wanafunzi wasioujua kusoma, kuandika na kuhesabu

Naye Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi.Christina Mndeme anatoa maagizo kwa walimu na maofisa elimu kuondoa tatizo la wanafunzi kumaliza elimu ya msigi wakiwa hawajui kusoma, kuhesabu na kuandika .

Wanafunzi waliomaliza Elimu ya Msingi Ruvuma hawajui Kusoma Wanafunzi waliomaliza Elimu ya Msingi Ruvuma hawajui Kusoma Reviewed by KUSAGANEWS on August 13, 2018 Rating: 5

No comments: