Nakuru, Kenya. Mtalii kutoka China, Chang Ming Chuang
amefariki dunia baada ya kuvamiwa na kiboko nchini Kenya,.
Mtalii huyo mwenye umri wa miaka 66 amefariki baada ya
kuvamiwa na kiboko alipokuwa akijaribu kumpiga picha
Taarifa kutoka Mamlaka ya hifadhi ya wanyama pori ya Kenya
imeandika kwenye mtandao wake wa tweeter kuwa raia huyo kutoka China alivamiwa
na kiboko wakati alipokuwa anampiga picha katika Ziwa Naivasha eneo la Sopa
Resort Nakuru
Taarifa hiyo iliongeza kwamba mwenzake waliyekuwa
wameongozana naye aliyefahamika kwa jina la Wu Peng Te mwenye umri wa miaka 62
alinusurika lakini bado yupo hospitali kwa ajili ya matibabu.
Ming Chuang alifariki alipokuwa akikimbizwa kwenye hospitali
ya wilaya ya Naivasha
Wananchi wa eneo hilo walilalamika wakisema kwamba viboko
hao huwavamia usiku kwani wakati huo macho yao huona zaidi kuliko mchana
Kwa mujibu wa mkazi wa kijiji, Safari Kadenge Karisa,
alisema idadi ya viboko imeongezeka wengi wao ikifika usiku huvamia wenyeji
kwenye makaazi yao
Alisema kwamba wanapotoa taarifa shirika la huduma la
wanyama pori wanachelewa kufika kwa ajili ya kutoa msaada
Mtalii atafunwa na Kiboko wakati akitaka kumpiga Picha
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment