Mbunge wa Liwale (CUF) Zuberi Kuchauka ametaja sababu
tatu za kurejea CCM
Akizungumza leo Jumatatu Agosti 13, 2018 katika ofisi
ndogo za CCM Lumumba jijini hapa baada ya kutambulishwa na Katibu Mkuu wa chama
hicho tawala, Dk Bashiru Ally, Kuchauka amesema moja ya sababu ni mgogoro ndani
ya CUF
Amesema sababu nyingine ni CCM kuwa na mabadiliko katika
kipindi cha miaka 10 iliyopita pamoja na utekelezaji wa ahadi mbalimbali za
uchaguzi
Kuchauka ametangaza kurejea CCM ikiwa zimepita siku
mbili tangu Julius Mtatiro, aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la uongozi CUF
upande unaomuunga mkono katibu mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad,
naye kuhamia CCM.
Katika
ufafanuzi wake Kuchauka amesema ndani ya CUF alijikuta katika wakati mgumu
kutokana na mpasuko hatua iliyoathiri utekelezaji wa majukumu yake ya kibunge.
“Sasa hivi
mtu akisema CUF unaulizwa ni CUF gani? Mtaona namna gani tulivyopoteza
mwelekeo, mimi nimechaguliwa na wananchi. Ukisimama kwenye jukwaa la CUF ya
Lipumba (Profesa Ibrahim-mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na ofisi ya msajili
wa vyama vya siasa) unaonekana msaliti,” amesema.
“Na
ukionekana jukwaa la CUF Maalim unafukuzwa kwenye chama. Kwa hiyo unakosa
utulivu na nikaona sina sababu ya kuendelea kubakia kwenye hali ya
wasiwasi.”
Katika
sababu yake nyingine Kuchauka amesema CCM ya sasa si ya mwaka 2005, ina
mabadiliko mengi.
“Ile ya
2005 ilikuwa inapoteza mwelekeo lakini CCM hii chini ya Rais Magufuli (John)
nimeikubali kwa kuwa inarejea kwenye misingi ya TANU. Mimi kama mpenda
maendeleo sikujutia kurejea,”amesema.
Amesema kutokana na mazingira hayo hakuona haja ya
kuchelewa kuchukua uamuzi wa kujiunga na chama hicho tawala.
“Kwa hivyo
mimi kama mbunge wa Liwale nikakuomba (Dk Bashiru) nije kwenye ofisi yako
nitamke kwamba kuanzia sasa hivi mimi si mwanachama tena wa CUF. Nyadhifa
nilizozipata nikiwa CUF zitakuwa zimeondoka,” amesema.<
Amesema sababu nyingine ni utekelezaji wa ahadi za
uchaguzi zilizotolewa na chama hicho tawala.
"Tumepata Sh1bilioni kwa ajili ya kujenga
hospitali, tumepata watumishi 80 wa afya. Kuna migogoro mingi, nimetembelewa na
mawaziri sita, watu walidhani wakichagua upinzani hatutatembelewa na
mawaziri," amesema
Mbunge CUF Ataja sababu za kujiunga na CCM
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 13, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment