Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde amewataka wawekezaji nchini kuacha
kutumia mawakala wanapotaka vibali mbalimbali
Waziri Mavunde
ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Agosti 13, 2018 wakati akizungumza kwenye
mkutano ulioandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) na wafanyabiashara
wenye asili ya China
Wawekezaji hao
walikuwa na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utendaji wa shughuli
zao hapa nchini
“Hakuna kibali
cha kufanya kazi au kuishi kinachotolewa zaidi ya siku 14, mnatumia mawakala
kuwaombea vibali ndiyo maana anapata majibu tofauti,” amesema Mavunde
"Nendeni
wenyewe kwenye ofisi husika na iwapo mmejaza fomu vizuri na mkaambatanisha kila
kinachohitajika na ikachukua zaidi ya wiki mbili njooni kwangu.”
Kuhusu muda wa
wageni kufanya kazi kabla ya kuwaelekeza wazawa shughuli husika na kuondoka,
Mavunde amefafanua kuwa ni suala la kisheria ambapo ikimalizika miaka mitano
anapaswa kuondoka
"Ipo
nafasi ya kukatiwa rufaa baada ya muda huo kama hiyo nafasi ni muhimu na hakuna
Mtanzania anayeweza kuifanya,” amesema
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Group Six International, Marco Lee amesema kuwa suala
la kuwasilisha vyeti vya taaluma wakati wa kuomba vibali vya kufanya kazi
nchini haoni kama lina maana
Amesema
anachofahamu wapo watu wana ujuzi na hawajasomea kazi husika, hivyo ni bora
waangalie ujuzi na uzoefu badala ya vyeti
Kwa upande
wake Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Dk Aggrey Mlimuka amesema kuwa watahakikisha
waajiri wa ndani na nje ya nchi wanazijua sheria za ajira na ndio maana
wameandaa mkutano huo.
Mavunde ataka wawekezaji kutotumia mawakala kuomba vibali
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 13, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment