Christopher Chiza (CCM) ameibuka mshindi katika uchaguzi wa
ubunge jimbo la Buyungu mkoani Kigoma baada ya kuwashinda wapinzani wake
wanane, akiwemo mgombea wa Chadema, Eliya Michael
Katika uchaguzi huo uliofanyika jana Jumapili Agosti 12,
2018, Chiza amepata kura 24,578 akifuatiwa na Eliya aliyepata kura 16,910
Akitangaza matokeo hayo leo Jumatatu Agosti 13 saa 11
alfajiri, msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo, Lusubilo Mwakabibi
amemtangaza Chiza kuwa mshindi
Vyama vingine na kura walizopata ni Demokrasia Makini (11),
UMD (12), NRA (17), UPDP (18), DP (22), AFP (51) na ACT – Wazalendo
kura 100
Mwakabibi amesema idadi ya waliojiandikisha kupigakura ni
61,980, waliopiga kura ni 42,356, kwamba kura halali zilikuwa
41,841 na zilizoharibika 515
Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, Chiza amesema yupo
tayari kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo na kuwaahidi utumishi uliotukuka
Amesema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji
ufumbuzi na akiapishwa ataanza nazo mara moja
Awali, Eliya amesema mawakala wake hawakuitwa kwenda
kujumlisha matokeo hayo, kubainisha kuwa uchaguzi huo ulikuwa na mazingira
magumu.
Amesema matokeo
aliyonayo kutoka katika kila kituo, hayafanani na yaliyotangazwa
“Kwa umri nilionao najiona mshindi wa uchaguzi huu,
nimejifunza mengi na umenijenga kwa kiwango kikubwa. Nimeshinda kwa kura za
watu ili wao wameamua kumtangaza mtu wanayemtaka,” amesema
CCM yashinda Buyungu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment