Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile
amekemea udhalilishwaji wa watoto ‘waliotelekezwa’ na baba zao ambao tangu jana
picha zao zimekuwa zikisambazwa katika mitandao ya kijamii baada ya kufika
ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakiwa na mama zao
Tangu jana wanawake waliotelekezwa na waume
zao wamefika katika ofisi hizo zilizopo Ilala jijini hapa, kuanza kusikilizwa
Katika ujumbe aliouandika katika ukurasa
wake wa mtandao wa Twitter akijibu maoni ya wachangiaji, Dk Ndugulile alivionya
vyombo vya habari kwa kushiriki kuonyesha picha za watoto katika mikusanyiko
hiyo, huku akitaka utaratibu ufuatwe katika kusikiliza mashauri ya walalamikaji
ikiwa ni pamoja na usiri
Mama wa mtoto wa Kichina afunguka
“Ni kosa kisheria kwa chombo cha habari au
mitandao ya jamii kuonyesha picha zenye kumdhalilisha mtoto kwa mujibu wa
sheria ya mtoto Namba 21 ya 2009. Navikumbusha vyombo vya habari kulinda haki
za watoto na kutokuwa washirika katika kudhalilisha haki za watoto,” alisema Dk
Ndugulile kupitia ujumbe wa Twitter
Akizungumza kwa njia ya simu Dk Ndugulile
amekiri kuandika ujumbe huo na kusisitiza kufuatwa kwa utaratibu wa kusikiliza
malalamiko ya kijamii
“Ushauri wangu kama Wizara inayosimamia haki
za watoto, suala kama hili linapaswa kufanyika kwa faragha, kwa sababu una deal
na watu na litakuwa endelevu,” amesema Dk Ndugulile
“Anachokifanya Makonda ni jambo zuri, lakini
linahitaji uangalifu na tufuate mifumo sahihi. Nitoe rai kwa wananchi wote
kufuata taasisi zinazohusika
Mwanaume apeleka malalamiko ya kunyanyaswa
na mke
Alipoulizwa sababu ya wananchi wengi
kujitokeza kwa mkuu wa mkoa kama ishara ya kuzidiwa kwa idara ya Ustawi wa
Jamii, Dk Ndugulile alikanusha
“Si kwamba Ustawi wa Jamii umezidiwa,
inawezekana wananchi hawana taarifa za kutosha kwa hiyo kupitia mikutano kama
hiyo watapata taarifa. Tufuate mifumo rasmi inayokubalika kisheria,” amesema.
Waziri akemea udhalilishaji watoto zoezi la Makonda
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 10, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment