Raisi Dokta John Magufuli ametoa shilingi Bilioni 10 kwa
ajili ya ujenzi wa nyumba za askari wenye vyeo vya chini ikiwa ni sehemu ya
kutatua changamoto zinazowakabili na kuwapa motisha ya kuendelea kufanya kazi
kwa weledi.
Amesema hayo jana wakati akihutubia katika ufunguzi wa
nyumba za askari na maonyesho ya kazi za polisi ambapo amewataka wabunge wote
nchini kusaidia kujenga nyumba za polisi kupitia fedha za jimbo kwani polisi
wanaishi maisha yasiyo mazuri hivyo wanapaswa kutambua jukumu lao.
Aidha Dokta Magufuli ametangaza ajira 1500 kwa askari
polisi waliotoka JKT ikiwa ni pamoja na kumtaka IGP Sirro kukaa na makamishna
wa jeshi hilo ili kuangalia askari wanaostahili kupandishwa vyeo nay eye atapitisha.
Pia amewataka askari polisi kutokatishwa tama ya maneno
ya kashfa na kebehi yanayosemwa dhidi yao kwani watanzania waliokuwa wengi
wanatambua na kuthamini kazi kubwa na nzuri wanayoifanya ya kulinda nchi.
Hata hivyo katika kuadhimisha siku ya Karume Raisi
Magufuli amewataka watanzania kuyaenzi maisha ya hayati Amani Abeid Karume kwa
kulinda Uhuru uliopo kudumisha amani pamoja na kuchapa kazi.
RAISI MAGUFULI ATOA BILIONI 10 KWA AJILI YA ASKARI POLISI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 07, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment