Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu
Lissu leo atafanyiwa upasuaji mwingine katika mguu wake wa kulia, hii ikiwa ni
mara ya 20 tangu alipoanza kutibiwa baada ya kushambuliwa kwa risasi mjini
Dodoma, Septemba mwaka jana
Akizungumza na Mwananchi jana ilipotaka
kujua maendeleo ya afya yake, Lissu alisema madaktari wamebaini bakteria katika
mguu wake wa kulia hivyo wameamua kumfanyia upasuaji ili kuwaondoa
“Kesho nitafanyiwa upasuaji katika huu mguu
wangu wa kulia ambao uliumizwa sana. Operesheni inafanyika baada ya madaktari
kubaini bakteria katika mifupa hivyo wamesema wakiunga bila kuwatibu bakteria
itakuwa ni tatizo,” alisema Lissu jana
Lissu, aliyeko nchini Ubelgiji kwa matibabu,
alifanyiwa upasuaji wa 19 Machi mwaka huu ikiwa ni mwendelezo wa matibabu
aliyokuwa akifanyiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopelekwa
akitokea Dodoma baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa nje ya
makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, mwaka jana
Lissu, ambaye pia ni rais wa Chama cha
Wanasheria Tanganyika (TLS), alisema baada ya upasuaji huo wa leo, utafuata
mwingine wa kuunga mfupa
“Niseme tu naendelea vizuri sana.
Ninawashukuru Watanzania kwa kunitibu, kwani wenye jukumu la kufanya hivyo
wamekataa lakini Watanzania hawajanitupa,” alisema.
Lissu kufanyiwa upasuaji wa 20
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment