Wakili ajitoa kesi ya kina Mbowe


Wakili Jeremiah Mtobesya anayewatetea viongozi tisa wa Chadema akiwamo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, amejitoa kwenye kesi hiyo

Mtobesya amechukua uamuzi huo leo Agosti 23 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri

Wakili huyo alijitoa kuwatetea washtakiwa hao mara baada ya Mahakama ya Hakimu Kisutu kuyatupilia mbali maombi yao ya kutaka kesi hiyo ya jinai namba 112 ya mwaka huu iahirishwe katika Mahakama ya Kisutu ili kusubiri   maombi yao na rufaa yaliyopo Mahakama ya Rufani yasikilizwe na kutolewa maamuzi

Hata hivyo Hakimu Mashauri aliyatupilia mbali maombi hayo kwa sababu kifungu cha sheria walichotumia cha 225 (1) (2) cha Mwenendo wa Mashauri ya Jinai Sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho2002 hakiipi mamlaka hayo

Viongozi hao tisa wanakabiliwa na mashtaka 13 ikiwamo  kuhamasisha maandamano Februari 16 mwaka huu siku moja ya uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kinondoni

Wakili ajitoa kesi ya kina Mbowe Wakili ajitoa kesi ya kina Mbowe Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: