Waandishi wa habari za jinsia nchini kesho watakabidhiwa
tuzo, katika kinyang'anyoro kilichoshirikisha vyombo vya habari 15, vilivyo
kubaliana kuandika habari kwa mlengo wa kijinsia
Waandishi hao watapewa tuzo hizo katika mkutano wa Jinsia na
Habari ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa kitengo cha Wanawake (UN
Women), unaoendelea jijini Dar es Salaam
Akizungumza leo Agosti 23, Mmoja wa Waratibu wa mkutano huo
na mtafiti kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa) Gladness Munuo
amesema tuzo hizo zinashindaniwa katika vipengere vitatu vya luninga,
magazeti na redio
"Tulikubaliana na vyombo vya habari juu ya kuripoti kwa
mlengo wa kijinsia, kwa maana ya kwamba hata wanapohojiwa watu watano basi
miongoni mwao wawepo wanawake," amesema
Munuo amesema bado suala la jinsia linahitaji msukumo hasa
wanawake ambao wengi wao hawapewi nafasi na hata wakuzungumziwa ni mwa mlengo
hasi na sio chanya
"Kwa hiyo hizi tuzo zitatoa msukumo kwa vyombo vyetu na
wanahabari kuona suala la jinsia ni la muhimu,"amesema
Waandishi wa habari za jinsia kupewa tuzo kesho
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 23, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment