Kesi mbili zilizosikilizwa katika mahakama tofauti dhidi ya
washirika wa zamani wa karibu wa Rais Donald Trump zimeibua vuta nikuvute ya
kisheria baada ya mmoja kukiri kuwa na hatia na mwingine kukutwa na hatia hivyo
kumweka matatani mkuu huyo wa nchi
Walioutikisa urais wa Trump ni meneja wake wa zamani wa
kampeni, Paulo Manafort ambaye amepatikana na hatia katika mashtaka manane kati
ya 18 ya udanganyifu wa kodi na masuala ya kibenki; na mwanasheria binafsi wa
zamani, Michael Cohen aliyekiri kuwa na hatia kwa mashtaka manane, yakiwamo
sita ya udanganyifu wa kodi na benki na mawili ya kufadhili kampeni za uchaguzi
kinyume cha sheria
Mbaya zaidi, mwanasheria huyo wa zamani wa Trump
aliithibitishia mahakama kwamba alikiuka sheria kwa maelekezo ya mgombea huyo
wa urais ambaye sasa ni Rais
Hili ni pigo kubwa kwa Trump baada ya kuhusishwa na mtu
ambaye alikuwa akimwamini kwa zaidi ya muongo mmoja. Cohen aliyeeleza kuwa ni
mtu wa karibu wa Trump alisema alikuwa akihusika kutatua matatizo yake
Kwa maelezo hayo, Cohen kwa hakika sasa anaweza kuwa chanzo
cha matatizo makubwa kwa Trump kwani alikiri kuwa alilipa dola za Marekani
130,000 na 150,000 kwa wanawake wawili ili kuwaziba midomo kuhusu uhusiano wao
na Trump kwa maelekezo ya mgombea huyo
“Rais alisema akiwa katika ndege ya Air Force One kwamba
hajui kuhusu muamala wa malipo ya dola 130,000, lakini sasa tunajua ukweli
kutoka kwa Michael Cohen, na tunaweza kusema kuwa Rais wa Marekani alidanganya
wananchi wa Marekani wakati alikuwa ndani ya ndege ya wananchi wa Marekani,”
mahakama ilielezwa
Hata hivyo, Cohen amekata rufaa katika mahakama ya Manhattan
dhidi ya madai yanayomkabili kwamba alikiuka sheria za uchaguzi na kudai kuwa
alifanya hivyo kwa maelekezo ya “mgombea”, kwa lengo la kuhakikisha uchaguzi
unakuwa salama
Katika kipindi cha miaka 10 ya utumishi wake akiwa
mwanasheia wa Rais, Cohen anadaiwa kuandaa malipo kwa mwigizaji wa filamu za
ngono, Stormy Daniels mwaka 2016
Mei mwaka huu, Trump alikiri kumpa Cohen fedha za malipo ya
kutaka kumnyamazisha mwigizaji huyo kuhusiana na suala la kuwa na uhusiano na
mlimbwende huyo siku kadhaa kabla ya kuanza kwa uchaguzi mkuu
Ingawa katika siku za karibuni, Trump amekana kufahamu
muamala wa malipo ya dola za Marekani 130,000 kama sehemu ya malipo ambayo
hayajabainishwa
Mwezi uliopita ilifahamika pia kuwa Cohen alimrekodi kwa
siri Trump walipokuwa wakijadiliana kuhusu ununuzi wa haki za umiliki wa mcheza
filamu za ngono, Karen McDougal ikiwamo hadithi yake kutoka kwa kampuni dada la
jarida la Enquirer
Malipo yafanywayo kwa siri kwa niaba ya mwanasiasa au
mgombea yeyote yanaweza kuchukuliwa kama ukiukwaji wa sheria za kampeni
Marekani
Urais wa Trump watikiswa mahakamani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 23, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment