Mabasi ya Shule yagongana uso kwa uso mmoja afariki


Mabasi mawili ya wanafunzi Shule ya Kivulini na Shule ya Nyamunge yamengana uso kwa uso  katika Barabara ya Mwanza – Simiyu katika eneo la Nane nane mkoani Mwanza na kusababisha kifo cha dereva na kujeruhiwa wanafunzi wanane wa shule hizo

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahamed Msangi, amesema aliyefariki katika ajili hiyo ni dereva wa basi la shule ya Nyamuge Albert Joram (58

Kamanda Msangi ambaye amehamishiwa makao makuu ya Jeshi la Polisi Dar es salaam, amesema katika ajali hiyo wanafunzi wanane na dereva wa  gari la shule ya Kivulini,  Kulwa Mayala (27), wamepata majeraha sehemu mbalimbali za miili yao hasa miguuni

“Majeruhi hao walikimbizwa katika kituo cha afya cha Buzuruga na baadae  mwanafunzi mmoja alilazimika kuhamishiwa hospitali ya rufaa, Bugando kwa matibabu zaidi huku wawili wakilazwa katika hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza,”amesema Kamanda Msangi.

Mabasi ya Shule yagongana uso kwa uso mmoja afariki Mabasi ya Shule yagongana uso kwa uso mmoja afariki Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: