Bobi Wine asomewa mashtaka ya uhaini


Baada ya Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine kufutiwa mashtaka na kukamatwa tena hatimaye amesomewa mashtaka yab uhaini

Wine alikamatwa muda mfupi baada ya mahakama ya kijeshi kumuondolea mashtaka ya umiliki haramu wa silaha nchini humo
Muda mfupi baada ya kuachiliwa huru, Wine alikamatwa tena na  kushtakiwa katika mahakama ya hakimu mkuu kujibu mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa

Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki  kwa jina maarufu Bobi Wine leo alifikishwa  katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda akitumia usafiri wa helkopta

Mawakili wake awali waliambiwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakoshikiliwa mjini Kampala
Kumekuwa na shinikizo kubwa kimataifa la kutaka Bobi Wine aachiwe huru

Bobi Wine asomewa mashtaka ya uhaini Bobi Wine asomewa mashtaka ya uhaini Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: