Agizo la JPM lamuingiza Mwenyekiti matatani.


MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Onesmo Maluda, amekamatwa na Jeshi la Polisi na kuswekwa ndani kwa tuhuma za ubadhirifu wa Sh. milioni 35

Agizo la kukamatwa kwa mwenyekiti huo ambaye pia ni diwani wa Kata ya Choma, lilitolewa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara  katika Kata ya Choma hivi karibuni

Aliagiza kukamatwa kwa viongozi wote wanaotuhumiwa kwa upotevu wa Sh. milioni 35 zilizotolewa na halmashauri ya wilaya hiyo kwa ajili ya ununuzi wa mashine ya kukoboa mpunga ya Kijiji cha Choma

Majaliwa alieleza kuwa mashine hiyo licha ya kununuliwa, ilifanya kazi kwa muda mfupi sana ikaharibika, hali iliyoleta sintofahamu kwa wananchi kutokana na baadhi ya viongozi kulalamikiwa kununua mashine mbovu

Waziri Mkuu alisema licha ya kulalamikiwa kwa ubovu, hata matengenezo yalishindikana

Akitoa taarifa baada ya kukamatwa kwa mwenyekiti huyo, Mkuu wa Polisi wilayani humo, Ally Mkalipa, alisema mwenyekiti huyo alikamatwa na kuunganishwa na watuhumiwa wenzake wanane kwa tuhuma za kuhusika na upotevu wa fedha hizo

Alisema polisi wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine akiwamo mkandarasi, Sadick Hans, ambaye alitoroka baada ya kusikia anatafutwa

Agizo la JPM lamuingiza Mwenyekiti matatani. Agizo la JPM lamuingiza Mwenyekiti matatani. Reviewed by KUSAGANEWS on August 23, 2018 Rating: 5

No comments: