TRA Arusha yawaonywa wafanyabiashara kwa kutotumia mashine za EFD



Mamlaka ya Kodi ya mapato(TRA) mkoa wa Arusha, imewataka wafanyabiashiara ,wakiwepo wamiliki wa Bar na nyumba za kulala wageni, kutumia mashine ya kielekroniki kwa kutoa risiti kwa wateja ili kuepuka kupigwa faini kati ya sh 3 milioni hadi 4.5 milioni kwa  watakaomatwa hawatumii mashine .

TRA mkoani hapa imeanza  msako  mchana na usiku katika maeneo yote ya mkoa wa Arusha ili kuwakatama wafanyabiashara ambao wamekaidi kutumia mashine za EFD.

Meneja wa TRA mkoa wa Arusha,Apili Mbaruku alitoa wito huo wakati anazungumza na Jumuiya ya wafanyabiashara mkoani Arusha,katika semina maalum ya kuwaelimisha juu ya matumizi ya mashine hizo za EFD.

Mbaruku alisema, kila bidhaa inayouzwa inapaswa kutolewa risiti, zikiwepo Bia hivyo, maafisa wa TRA watafanyakazi usiku na mchana kuhakikisha wafanyabiashara wote ambao wanahitajika kutumia mashine hizo wanatumia.

"hatupendi kuwapiga faini lakini italazimika kufanya hivyo, kwani tunasimamia sheria na imeonekana idadi kubwa yawafanyabiashara mkoani hapa hawatumii mashine za EFD kama ambavyo inatakiwa"alisema

Awali, Msimamizi mkuu wa mradi wa matumizi ya EFD mkoani Arusha, Alphael Mollel alisema, maafisa wa TRA mkoani Arusha, wameanza msako kwa ambao hawatumii mashine na wasilaumiwe kwa kazi hiyo.

"tayari tumeanza kukamata watu, wanakuja ofisini wanalia lakini, tunawaambia hakuna jinsi lazima walipe faini milioni 3 ama milioni 4.5 hindwa tutachukuwa hatua ikiwepo kufunga biashara "alisema

Meneja Huduma kwa Wateja wa TRA Arusha, Regina Mkumbo alisema, mkoa wa Arusha kuna mawakala zaidi ya 10 ambao wanauza mashine za EFD hivyo, hakuna sababu ya afanyabiashara kushindwa kununua kwa wakati.

Hata hivyo, alisema kwa ambao mashine zao zimeharibika wanapaswa kutoa taarifa TRA kwa barua na sehemu waliyonunua mashine ili kuhakikisha hawapigwi faini kwa kutotumia mashine.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Arusha, Locken Adolf aliwawaka wafanyabiashara kufuata sheria ili kuondoa migogoro na serikali, kwani tayari sheria ya matumizi ya lazima ya EFD imepitishwa.

"ni ukweli jambo hili limekaa pabaya lakini hatuna jinsi lazima tutumie mashine kwani pia zinasaidia kutunguza makadilio makubwa ya kodi ambao tumekuwa tukifanyiwa"alisema.



TRA Arusha yawaonywa wafanyabiashara kwa kutotumia mashine za EFD TRA Arusha yawaonywa wafanyabiashara kwa kutotumia mashine za EFD Reviewed by KUSAGANEWS on July 09, 2017 Rating: 5

No comments: