MANISPAA MOROGORO WAFUNGIA NDANI WATEJA MAHOTELINI WAKIDAI 'HOTEL LEVY



WAFANYABIASHARA wa mahoteli na nyumba za kulala wageni manispaa ya Morogoro juzi pasipo taarifa yoyote wamejikuta wakipoteza mapato yao yanayokadiriwa kufikia shilingi mil.200 baada ya halimashauri hiyo kudaiwa kujichukulia sheria mkononi na kuzifunga kwa makufuri hoteli na gesti zaidi ya 20.

Baadhi yao wakiungwa mkono na viongozi wao akiwemo Katibu wa chama-MOGOA, Mtei Mtei walisema zoezi hilo lililofedhesha kazi zao hizo lilianza 6.Julai asubuhi kwa maofisa waliojitambulisha kutoka Manispaa hiyo kufika sehemu zao za biashara na kuzifunga makufuli milango yote kwa madai hawajalipa tozo ya hoteli ‘Hotel levy’.

“Tumeshangazwa na tozo hii,kwanza ilishafutwa na Tamisemi tangu mwaka 2013na halmashauri kuagizwa kukaa na sisi ili kuona namna ambavyo tutaiwezesha halamashauri kupata fedha na tulisha kubaliana asilimia 10 ya pato kwa mwaka badla ya 20 ya awali” alifafanua wafanya biashara mmoja.

Kwa upande wake katibu wa Mogoa, Mtei alisema kimsingi wakotayari kulipa tozo waliyokubaliana kuiongezea halmashuri pato kwa mwaka ila yenyewe imekuwa haitaki maelewano na wao jambo ambalo limewasababishia kufikishana mahakamani dhiidi ya mambo hayo.

Katika ufafanuzi wake katibu huyo alisema wafanya biashara hao wamefedheheka baada ya baadhi ya hoteli kufungiwa milango huku zikiwa na wageni,huku hoteli na nyumba nyingine za kulala wageni zikishindwa kuendeleza maombi zilizokuwa zimepata kutoka kwa wateja wao wanao waamini.

“unajua kipindi hiki ni cha mzunguko mkubwa wa fedha wazazi wanapeleka watoto mashuleni hivyo wanalazimika kulala mjini,kuna watalii na Mikumi,Udizungwa na Serous wamekosa huduma,kuna bokingi za kumbi kwa sherehe na mikutano ambapo pia walipaswa kulisha washriki,hayo yote na mengineo fedha tumepoteza”alifafanua Mtei.

Hata hivyo alisema kwa sasa chama kimewashuri waathirika mmoja mmoja kumfungulia mashitaka Mkurugenzi wa Manspaa hiyo sambamba na kuitaka mahakama kutafsiri sheria juu ya nani mwenye mamlaka ya kufunga shuguli ya mtu kisheria.

Alipotafutwa mkurugenzi wa manspaa hiyo John Mgalula hakupatikana ofisini kwake na hata alipotafutwa kwa simu yake ya kiganjani pia haikuwa na majibu yoyote,hata hivyo Meya Paschal Kihanga alikana kuwepo kwa zoezi bila taarifa akisisitiza kuwa hilo ni agizo la kamati ya fedha mwishoni mwa wezi uliopita likiwataka watendaji kukusanya madeni yote.

“sikwepo kwa muda mrefu na nikili kuwa zoezi hili binafsi silifahamu vema na sikweli kuwa linafanyika bila taarifa isipokuwa ninachokumbuka ni kuwa mwishoni mwa mwezi uliopita kwenye kamati ya fedha tulimwagiza mkurugenzi kukusanya haraka madeni yote ya fedha zilizo nje…inawezekana huo ndio utekelzaji wake”alifafanua Kuhanga.



MANISPAA MOROGORO WAFUNGIA NDANI WATEJA MAHOTELINI WAKIDAI 'HOTEL LEVY  MANISPAA MOROGORO  WAFUNGIA  NDANI WATEJA MAHOTELINI WAKIDAI 'HOTEL LEVY Reviewed by KUSAGANEWS on July 09, 2017 Rating: 5

No comments: